Wednesday, June 6, 2012

ALICHOSEMA RONALDO KUHUSU KUBAKI REAL MADRID.

Posted: 5th June 2012 by MillardAyo in News
0
Cristiano Ronaldo akiwa kwenye bata.
Mchezaji staa wa Real Madrid Cristiano Ronaldo ameweka wazi kwamba anatamani aendelee kuichezea club hiyo kwenye maisha yake yote ya soka yaliyobaki.
Gazeti ya Uingereza (The Sun) limeandika kwamba Ronaldo amesema kama ingekua ni uwezo wake angesaini hata mkataba wa miaka kumi wa kuichezea club hiyo ila hilo linashindikana kwa sababu kuna taratibu zilizowekwa na club.
Ronaldo ambae anajiandaa na Euro 2012 mpaka sasa ameshaifungia Real Madrid magoli 112 toka ajiunge nayo mwaka 2009 ambapo inakua club ya kwanza yeye kuifungia magoli mengi toka aanze soka, aliifungia Manchester United magoli 84 wakati alipoichezea kuanzia 2003-2009.
6
Mkali wa Basketball Hasheem Thabeet kwenye interview na Millard Ayo wa AMPLIFAYA Clouds FM.
.
.
0
Nicki Minaj, Cam'ron na Foxy Brown.
Baada ya mtangazaji wa kituo cha radio cha Hot 97 New York Marekani Peter Rosenberg kupanda kwenye stage ya tamasha kubwa la Summer Jam na kutoa maneno ambayo yalionekana kumlenga Nicki Minaj kwa hiphop ya biashara anayoifanya, Nick Minaj ameamplfy sababu zilizomfanya agome kupanda kwenye stage kuperform baada ya kusikia hiyo kauli.
Nicki amesema hayo maneno yalionekana wazi kabisa kumvunjia heshima kwa sababu mtangazaji huyo pamoja na kumponda Nicki alitaja kabisa na jina la wimbo wa Nicki wa Starships ambapo alisema tuko hapa kwa ajili ya real hiphop, yani hiphop ya ukweli kwa hiyo kama umekuja hapa kusikiliza nyimbo kama starships hatuko hapa kwa ajili yako na anaefanya hiphop isiyo real siongei nae.
Peter Rosenberg mtangazaji wa HOT 97.
Baada ya hiyo statement Lil wyne ambae ni boss wa Nicki Minaj alimkataza Nicki kupanda kwenye stage kwa sababu ilikua ni statement ya kuivunjia heshima YMCMB, na baadae Nicki akasema hakuna atakaeivunjia heshima YMCMB Young Money Cash Money.
Lil Wyne alipomkataza Nicki kupanda kwenye stage, aliwakataza na wasanii wengine wote wa YMCMB na wasanii wengine ambao wangepanda nao kwenye stage wakagoma japo sio YMCB.
Kwenye interview ya leo, Nicki Minaj amesema hata kama angeperform asingeperform single ya Starships kwa sababu hiyo consert ya hot 97 ilikua ya hiphop, kwenye usiku huo alikua apande kwenye stage na Beenie Man, Foxy Brown na Cam’ron.
Nicki Minaj amesema anaelewa kwamba inawezekana Peter alikua anatania lakini ikachukuliwa kama ni diss, ila alipaswa kuomba msamaha au kurekebisha lakini hakufanya hivyo, pamoja na hayo Nicki amekiri kwamba atafanya show ya bure kwa watu wake wa New York ambao hawakumuona kwenye consert ya Summer Jam.
Wengine wa Cash Money ambao walitakiwa kuperform kwenye hiyo show lakini hawakuperform japo walikua backstage ni pamoja na Busta na Dj Khaled.……….. hizo hapo chini ni Tweets zilizoandikwa baada ya mtangazaji huyo wa hot 97 kumdiss Nicki Minaj.

 


No comments:

Post a Comment