Siku tatu za maombolezi ya Saitoti
Kenya
imetangaza siku tatu za maombolezi baada ya kifo cha Waziri wa Usalama
wa Kenya, Profesa George Saitoti, na naibu wake, Orwa Ojode, kwenye
ajali ya helikopta ya polisi katika eneo la Ngong, nje ya Nairobi.
Rais
Mwai Kibaki alisema kifo cha Bwana Saitoti ni msiba mkubwa kwa taifa,
na serikali imetangaza kuwa baraza la mawaziri litakutana Jumatatu,
kujadili tukio hilo.
Idara
ya polisi imesema uchunguzi utafanywa kujua sababu ya ajali hiyo, na
balozi wa Marekani mjini Nairobi, amesema Marekani iko tayari kusaidia
kwenye uchunguzi huo, ikiwa itatakiwa kufanya hivo.
Msemaji wa polisi alieleza kwamba inavoelekea kuanguka kwa helikopta hiyo lilikuwa tukio la ajali.
Raia
wa Kenya walikuwa na masikitiko Jumapili, baada ya taarifa ya ajali
hiyo kujulikana, na watu wamekuwa wakizuru nyumba ya kuhifadhi maiti
mjini Nairobi kutoa heshima zao.
Makamo
wa rais wa Kenya, Kalonzo Musyoka, alipofika kwenye tukio la ajali
alitoa rambi-rambi zake na alieleza wale waliokuwamo ndani ya ndege
ambao wote wameteketea:
"Ndege
hiyo ya aina ya Eurocopter ya police airwing, ambayo ilikuwa inaelekea
Yugis, ilikuwa imembeba Waziri George Saitoti, naibu waziri Orwa Ojode
na maafisa rubani wa ndege, Nancy Gitwanja na Luke Oyugi, na vilevile
askari wawili ambao wanakuwa wanaandamana na Waziri Saitoti, Inspector
Tonkei na Thomas Murimi"
Rambi-rambi
zimekuwa zikimiminika nchini Kenya, pamoja na za Kofi Annan, Katibu
Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, ambaye alipatanisha baada ya ghasia
za uchaguzi uliopita nchini kenya.
Profesa
Saitoti alikuwa akizungumza kwa ukali dhidi ya al-Shabaab na
inaaminiwa alihusika na uamuzi wa jeshi la Kenya kuingia Somalia mwaka
jana.
Bwana
Saitoti aliwahi kuwa makamo wa rais na waziri wa fedha katika serikali
ya Rais Moi, na akitarajiwa kugombea urais katika uchaguzi wa mwaka
ujao.
Alikuwa na umri wa mika 67
BAISKELI ZINAVYORAHISISHA MAISHA YA WANAWAKE WILAYANI RUFIJI
Akina mama wakitumia baiskeli kwenda kutafuta riziki katikamji wa Ikwiriri Rufiji, mkoani Pwani jana. Picha zote na Kamanda Mwaikenda
SASA IKWIRIRI IKO SHWARI BAADA YA KASHESHE KUMALIZIKA
Mji
wa Ikwiriri, wilayani Rufiji, Pwani, ukiwa shwari baada ya sakata la
mapigano ya wakulima na wafugaji lililosababishwa na Polisi na hatimaye
kumalizika hivi karibuni. Watu kadhaa walipoteza maisha katika sakata
hilo. PICHA NA KAMANDA MWAIKENDA
Ajali ya nyingine ya magari kati ya Rav 4 na Fusso yatokea Mbeya.
Gari la Fusso lililo sababisha Ajali hiyo
Namba za gari la Fusso
Toyota Rav 4 ikiwa imebamizwa vibaya na Fusso hilo
Gari la Rav 4 lilivyo haribika kwa nyuma
Namba za Gari la Rav 4
Fusso kwa nyuma
Fusso kwa Mbele
***********************************
Ajali Mbaya imetokea usiku huu iiyo husisha Gari la Fusso namba T 596 BUB pamoja na Rav 4 namba
T 675 ATK, Maeneo ya CCM Mkoani Mbeya.
Shahidi
aliye kuwepo eneo la tukio amedai ya kuwa Dereva wa Gari la mizigo
Fusso alikuwa mwendo kasi sana, na huku akijaribu kuyapita magari
mengine matano ambayo yalikuwa mbele yake. Wakati huo anaendelea
kuyapita magari hayo tayali dereva wa Rav 4 alikuwa amesha washa taa
kuonesha kuwa anaelekea kulia na ndipo Dereva wa fusso akaligonga Gari
la Rav 4 ambalo baada ya hapo liliseleleka kwa umbali wa Takribani mita
300 kutoka usawa wa sehemu ambapo liligongewa.
Hata hivyo dereva wa Fusso aliyesababisha Ajali hiyo amekimbia eneo hilo. Hakuna aliye umia wala kupata majeruhi.
JK AWAAPISHA MABALOZI 10
Rais Dkt.Jakaya Kikwete ashiriki kumuaga Muasisi wa CHADEMA Bob Makani katika viwanja vya Karimjee leo
Rais Jakaya Kikwete akiteta jambo na mwenyekiti wa chama cha CHADEMA Mh. Freeman Mbowe wakati wa kuaga mwili wa Muasisi wa chama cha CHADEMA marehemu Bob Makani |
Rais Dkt.Jakaya Kikwete, Makamu wa Rais Dkt.Mohamed Gharib Bilal na Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe wakibeba jeneza la marehemu Bob Makani |
Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitoa heshima za Mwisho |
Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiteta jambo na mjumbe wa tume ya kukusanya maoni juu ya katiba Prof.Mwesiga Baregu katika viwanja vya Karimjee leo. |
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimpa pole Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Wilbroad Slaa katika viwanja vya Karimjee kufuatia msiba wa muasisi wa Chama hicho Bob Makani |
TAIFA STARS, GAMBIA ZAINGIZA MIL 124/-

Mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia Kanda ya Afrika kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Gambia (The Scorpions) iliyochezwa Juni 10 mwaka huu Uwanja wa Taifa, D ar es Salaam imeingiza sh. 124,038,000.
Mapato
hayo yametokana na washabiki 31,122 waliokata tiketi kushuhudia
pambano hilo kwa viingilio vya sh. 3,000, sh. 5,000, sh. 10,000, sh.
20,000 na sh. 30,000. Washabiki 25,901 walikata tiketi za sh. 3,000.
Asilimia
18 ya mapato hayo ambayo ni sh. 18,921,050.85 ilikwenda kwenye Kodi ya
Ongezeko la Thamani (VAT) wakati gharama kabla ya mgawo zilikuwa
tiketi (sh. 6,555,000), bonasi kwa Taifa Stars (sh. 15,767,542.37),
waamuzi (sh. 13,372,000), usafi na ulinzi (sh. 2,350,000), maandalizi
ya uwanja- pitch preparation (sh. 400,000), Wachina- Beijing
Construction (sh. 2,000,000), umeme (sh. 300,000) na mafuta ya jenereta
(sh. 200,000).
Kwa
upande wa mgawo asilimia 20 ya gharama za mechi ni sh. 12,834,481,
asilimia 10 ya uwanja sh. 6,417,241, asilimia 5 ya Shirikisho la Mpira
wa Miguu Afrika (CAF) sh. 3,208,620, asilimia 20 ya Mfuko wa Maendeleo
ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 12,834,481 na asilimia 45 ya TFF (sh.
28,877,583).
Rais Kikwete na Mama Salma Wakagua mahindi Shambani kwao kijijini Msoga
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakikagua
mahindi shambani kwao kijijini Msoga,Chalinze,wilayani Bagamoyo wakati
wa mapumziko ya mwisho wa wiki(picha na Freddy Maro)
WAZIRI MKUU PINDA AFUNGUA KIWANDA CHA NYUKI KIBAHA
JK AMWAPISHA KATIBU TAWALA MKOA WA RUVUMA, APOKEA KITABU CHA SIMULIZI ZA WAKWERE
Katibu
Tawala mpya wa mkoa wa Ruvuma Bwana Hassan Mpapi Bendeyeko akila kiapo
mbele ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam leo
asubuhi.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Taaluma za Kiswahili TATAKI Dkt.Aldin Mutembei akimkabidhi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kitabu cha kwanza cha fasihi simulizi ya jamii ya Wakwere ikulu jijini Dar es Salaam leo.Kulia anayeshuhudia ni Mkuu wa Idara ya historia katika chuo kikuu cha Dar es Salaam Profesa Kapepwa Tambila. Dkt.Mutembei ambaye pia ni mchapishaji na msimamizi wa tafiti za Tamaduni lugha na fasihi za makabila ya Tanzania alikabidhi pia kamusi Asisi ya Kiingereza-Kiswahili na Kiarabu(picha na Freddy Maro).
Mkurugenzi wa Taasisi ya Taaluma za Kiswahili TATAKI Dkt.Aldin Mutembei akimkabidhi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kitabu cha kwanza cha fasihi simulizi ya jamii ya Wakwere ikulu jijini Dar es Salaam leo.Kulia anayeshuhudia ni Mkuu wa Idara ya historia katika chuo kikuu cha Dar es Salaam Profesa Kapepwa Tambila. Dkt.Mutembei ambaye pia ni mchapishaji na msimamizi wa tafiti za Tamaduni lugha na fasihi za makabila ya Tanzania alikabidhi pia kamusi Asisi ya Kiingereza-Kiswahili na Kiarabu(picha na Freddy Maro).
No comments:
Post a Comment