Mchezaji wa Chelsea Fernando Torres jana ameifungia timu yake ya taifa ya Hispania magoli mawili kwenye mechi na Ireland ndani ya mzigo wa Euro 2012.
Torres amesisitiza kwamba hana noma kama kocha wa timu ya taifa atamuweka benchi kwenye mechi yao ya mwisho ya makundi dhidi ya Croatia, anasema yeyote anaweza kucheza kwa sababu kikosi kina wachezaji wakali kwa hiyo kukaa benchi sio ishu.
Torres alichezeshwa dakika chache sana kwenye mechi ya kwanza dhidi ya Italy ila jana kocha alimpa muda wa kutosha ambapo alionyesha ujazo wake kwa kulifungia taifa lake magoli mawili kwenye hiyo mechi ambayo walishinda nne bila ushindi ambao umeiweka Hispania kileleni kwa kufuzu kuingia kwenye mtoano.
Kocha wa zamani wa Chelsea Andre Villas-Boas amejitokeza kama mmoja wa makocha wanaogombania nafasi ya kuifundisha Tottenham baada ya club hiyo kumfukuza Harry Redknap.
Kocha huyo mreno ambae sasa hivi hana kazi toka february mwaka huu inaaminika kwamba kuna uwezekano mkubwa wa yeye kupata hiyo nafasi baada ya kupata support ya kampuni ya sky bet inayoshughulika sana na ishu za mpira ambao inasemekana jana baadhi ya wakurugenzi wa club hiyo waliwasiliana na villa boas.
Tottenham inamtafuta mrithi wa kocha Harry Redknap ambae ameifundisha club hiyo kwa miaka minne kabla ya kufukuzwa juzi jumatano, Kocha wa Everton David Moyes na kocha wa Wigan Roberto Martinez wanatajwa pia kwamba wako kwenye hiyo list ya kumchagua mmoja wa kuifundisha tottenham, lakini pia mchezaji wa zamani wa Tottenham Jurgen Klinsmann yuko kwenye hiyo list inayotajwa na vyombo vingi vya habari.
Huyo ni Shafie Dauda |
EXCLUSIVE INTERVIEW NA MTOTO WA HASSAN AFIF ANAYECHEZA TIMU MOJA NA RAUL GONZALEZ
Nimepata kuongea mengi na Ally endelea kufuatilia shaffihdauda.com
UCHAGUZI WA VIONGOZI WA YOUNG AFRICANS SPORTS CLUB (YANGA)
Kamati
ya Uchaguzi ya TFF inawataarifu wadau na wapenzi wa soka kuwa mchakato
wa uchaguzi wa viongozi wa YANGA kujaza nafasi zilizowazi za Kamati ya
Utendaji unaendelea vizuri chini ya Kamati ya Uchaguzi ya YANGA.
Kamati
ya Uchaguzi ya TFF imepokea kutoka Kamati ya Uchaguzi ya YANGA nakala
za fomu za maombi ya uongozi wa YANGA pamoja na nakala za vyeti vya
elimu vya waombaji uongozi kama sehemu ya taarifa ya awali ya mchakato
wa uchaguzi huo wa YANGA. Kamati ya Uchaguzi ya TFF imebaini kuwa baadhi
ya waombaji uongozi wamewasilisha nakala za vyeti vya kuhudhuria masomo
ya sekondari (Secondary School Leaving Certificate) badala ya nakala za vyeti vya kuhitimu masomo ya elimu ya sekondari (Certificate of Secondary Education).
Kamati
ya Uchaguzi ya TFF imekwisha ielekeza Kamati ya Uchaguzi ya YANGA
kuwataka wagombea wote kuzingatia Kanuni za Uchaguzi za wanachama wa TFF
Ibara ya 10(4) na (5) inayowataka wagombea wote kujaza Fomu Na.1 ya
maombi ya uongozi na kuambatanisha nakala ya cheti cha Elimu ya Sekondari (Certificate of Secondary Education)
kama ilivyoainishwa kwenye Fomu Na.1 kipengere Na.9. Kamati ya Uchaguzi
ya TFF imeiagiza Kamati ya Uchaguzi ya YANGA iwashauri wagombea ambao
vyeti vyao vimepotea wawasiliane na Baraza la Mitihani la Tanzania
(NECTA) kwa maandishi ili kupata ‘Statement of Examination Results’ itakayotumwa kwa Kamati ya Uchaguzi ya YANGA kupitia TFF kuthibitisha kuwa wamehitimu elimu ya kidato cha nne.
Uhakiki wa
vyeti vya elimu ya sekondari vya waombaji uongozi hufanywa na NECTA na
vyuo husika kwa elimu ya juu kwa chaguzi za wanachama wa TFF. Wanachama
wote wa TFF wanatakiwa kuzingatia kikamilifu matakwa ya Kanuni za
Uchaguzi.
Imetolewa na:
IDARA YA HABARI
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
SHOMARY KAPOMBE MWANAMICHEZO BORA WA MWAKA 2011
TUZO ZA TASWA ZILIVYOFANA USIKU HUU DIAMOND JUBILEE
![]() |
Rais wa TFF, Leodegar Tenga wa pili kulia akiwa na Jellah Mtagwa kushoto kwake |
![]() |
Familia ya ndondi |
![]() |
Wadau wa ndondi |
![]() |
Tedi Mapunda kulia na bosi wake |
![]() |
Eiphraim Mafuru kulia |
![]() |
Maswahiba wa siku nyingi, Shaaban Mkongwe kulia akiwa Waziri Mahadhi |
![]() |
Beki wa Mtibwa Salum Swedi 'Kussi' |
![]() |
Kaburu kulia akikabidhi tuzo |
![]() |
Daud Salum 'Bruce Lee' kulia akikabidhi tuzo |
![]() |
Athumani Hamisi akikabidhi tuzo |
![]() |
Asha Baraka akikabidhi tuzo |
![]() |
Mafuru akikabidhi tuzo |
![]() |
Ridhiwani Kikwete kulia akiwa na Benny Kisaka kushoto, cheko la maana |
![]() |
Dioniz Malinzi kushoto akikabidhi tuzo |
![]() |
Kapombe akipokea tuzo ya Mwanamichezo Bora Chipukizi kutoka kwa Salim Amir |
![]() |
Mzee Matumla akimkabidhi Kaburu tuzo ya Emmanuel Okwi |
![]() |
Mwenyekiti wa RT, akimkabidhi tuzo Mwanahamisi Gaucho |
![]() |
Aggrey Morris kushoto akipokea tuzo ya Mwanasoka Bora wa mwaka |
![]() |
Ally Choky akikabidhi tuzo |
![]() |
Mafuru akipakia msosi |
![]() |
Kim Poulsen kulia akiwa na nani sijui |
![]() |
Jamal Rwambow kulia na Kaburu wakati wa maakuli |
![]() |
Serengeti Beer inapokolea, mambo huwa hivi... |
![]() |
Mzee El Maamry akimkabidhi tuzo George Tarimo |
![]() |
Mzee Mwinyi akimkabidhi tuzo Adolph Rishard |
![]() |
Mzee Mwinyi akimkabidhi tuzo Peter Tino |
![]() |
Mzee Mwinyi akikabidhi tuzo |
![]() |
Waziri Mahadhi akimpokelea tuzo marehemu baba yake, Omar Mahadhi |
![]() |
Kaburu akimsaidia Kapombe kupokea tuzo ya Mwanamichezo Bora wa mwaka 2011 |
![]() |
Juma Pinto akikabidhi tuzo |
![]() |
Zena Chande na swahiba zake |
![]() |
Shaffih Dauda kulia, Amour Hassan na Michael Maluwe |
![]() |
Tullo Chambo na bosi wake |
![]() |
Akina nani sijui hawa |
![]() |
BIN ZUBEIRY kulia na Shaffih Dauda |
No comments:
Post a Comment